Home
About Us
Photo Gallery
Home
Planner
Planner
Cake/Keki
Clothings/Mavazi
Decoration/Mapambo
Drinks/Vinywaji
Food Caterers/Chakula
Gift centers/Zawadi
Honeymoon/Fungate
Invitation card/Kadi za mwaliko
Live bands
MC/Mwendesha Shughuli
Music/Muziki
Saloon/Beauty Clinic/Spa
Still Picture/Picha za mnato
Transportation/Usafiri
Trumpets/Tarumbeta
Venues/Kumbi
Videos/Video
Wedding planners
Wedding rings/Pete
   
Create Email List
Online Pledges
Create Free Website
Track your Payments
Budgeter Advisor
 
   
10 things while chosing a photographer

Jinsi ya kuchagua mpiga picha, vitu 10 vya kuzingatia

Ndio siku yako kubwa, pamoja na mambo mengine yote yanayoendelea, unataka siku ya mwisho uwe na kumbukumbu bora ya siku hiyo, hapa ninamaanisha picha za mnato na picha za video. Ni kwasababuu hiyo basi kwamba ni muhimu ukachagua mpiga picha na kemera man wazuri ambao watakutendea haki na kazi yako. Na pengine hujui ni jinsi gani utabaini mpiga picha na kemera man wa kaliba hiyo, na hapa chini ndio natoa dokezo.

Kupiga picha za mnato na zile zinazotembea ni taaluma mbili zinazorandana ila hapa nitaongelea uchaguzi wa mpiga picha za mnato. Cha muhimu unataka matukio muhimu katika harusi yako yakamatwe barabara, zingatia:

 

1.       Umependezwa na kazi za awali za huyu mtu?

Kabla hata hujaanza kumfikiria huyo mpiga picha, hakikisha umeona kazi zake alizofanya awali, yaani wanakamati wanaweza kupendekeza watu kadhaa, sio mara zote huwa ni kutokana na ubora wa kazi za hao watu, saa nyingine huwa ni…kwahiyo sisitiza kukutana nao wakiwa na kazi zao, mara nyingi wapiga picha bora watakua na album ambazo wameweka kazi zao bora zaidi.

 

Je unaridhishwa na ubora wa kazi yake? Picha zake zinamvuto kwako? Mwanga na rangi katika picha zinavutia? Je style yake ndio unayoifikiria kwa picha zako? Kuna aina Fulani mahususi ya picha unataka na je ana uwezo wa kupiga picha za aina hiyo? (Maharusi wengi huenda kwenye professional houses kupiga picha hizi). Usiridhike na mmoja jaribu kuangalia kazi mbili tatu, kama hujaridhishwa basi hamna haja ya kumfikiria zaidi.

 

Sasa basi, kuna mtindo, hasa kama mpiga picha anatokea kwenye studio au kampuni, ukaongea na mtu mwingine au ukaoneshwa picha za mpiga picha mwingine ila siku ya siku ukaletewa mtu mwingine. Onesha tangu mwanzo kwamba hautaentertain ujinga huo, kuwa mjanja kufahamu jina la mpiga picha tangu mwanzo na kusisitiza kuwa ndiye utakayemtegemea siku hiyo, fanya malipo ya awali na kubali kutoa malipo ya mwisho mara tu baada ya kupokea kazi yako na kuridhishwa nayo.

 

2.       Ana uzoefu wa kiasi gani?

Kama nyongeza ya hapo juu, huyu mpiga picha ana uzoefu wa kiasi gani katika upigaji picha za harusi na shughuli kama hizo? Uzoefu unasaidia kwani mpiga picha huyu ana uwezo wa kujua au kuotea ni matendo gani yatatokea, wakati gani yatatokea na hivyo kuwa tayari kuyakamata, mgeni katika upigaji picha wa shighuli hizi ataishia kukimbia kimbia kufuata matukio anaposikia labda MC kasema kitu na kuyakosa yote kwa kutokua positioned at the right place at the right time.

 

Mimi ni mmoja wa wale wanaochallege kutopata kazi kutokana na ukosefu wa experience, sasa bila kupewa kazi hiyo experience itatoka wapi? Kama umependezwa na kazi za mpiga picha ambaye bado hajapata uzoefu wa kutosha na shughuli hizi, unaweza kumsaidia kwa kumpatia orodha ya matukio muhimu ambayo wewe unataka yakamatwe, mtiririko wa matukio katika siku hiyo na sitting arrangement ya wageni wako, kwa jinsi hii atakua tayari zaidi na kufanya kazi yake kwa ufanisi. Plus utakua umemuongeze uzoefu, good for you.

 

Uzuri mmoja wa kuwa na mtu mzoefu ni kwamba ukiacha mambo ya ratiba, anaweza kupredict and anticipate things that could wrong na anakua prepared kudeal navyo.

 

3.       Yuko tayari kutoa kemera ngapi?

Mpiga picha mmoja kusema kweli huwa hatoshi kucover event nzima peke yake, wapiga picha wajanja wenye kujua kazi yao huja na team ya watu kadhaa, kamera walau mbili au tatu kutokana na ukubwa wa sherehe, na wengine wanakua ni technical guys, taa, stands na vitu kama hivyo. Je mpiga picha wako ana timu yake? Huyu ni Yule ambaye umemchuja katika awamu hizo mbili hapo juu, so hao kemera man wengine watakua ni jukumu lake kuhakikisha ubora aliokuahidi. Itabidi tu uassume kwamba kazi nzuri ulizoona kwa album ni matokeo ya yeam work hiyo hiyo atakayokuahidi. Usijidanganye ati atafanya kazi yote mwenyewe. Kama ndio hivyo huu ndio muda wa kumdrop huyu hata kama amefaulu hatua nyingine.

 

4.       Anafanya kazi na Mpiga picha za video?

Mara nyingine hawa watu wawili huwanya kazi kama team pia, je mpiga picha wako anafanya kazi na mpiga picha za kutembea (moving picture), hii itakua vema kwako kwani ukipata package hii inamaanisha savings on your side, lazima ilete maana, kama ukipata video man mwingine na gharama zao pamoja zikawa pungufu zaidi then kuwa huru kutafuta video man mwingine. Inabidi uwe makini usije uakasettle for this deal wakati video man ni bogus, makala nyingine itaeleza jinsi ya kuchagua video man.

 

5.       Wanaweza kufanya kazi pamoja?

Kama anafanya kazi solo je ana uwezo wa kufanya kazi na video man mwingine? Yani wakafanya kazi kwa kushirikiana, usije ukaishia kuwa na mataa kumi, tano za video man tano za kamera man mpaka wakakuharibia ambiance ya siku yako, nyaya zinapishana kila mahali. So hakikisha kuwa hawa wawili hata kama hawafahamiani watakua tayari kukaa pamoja na kuplan jinsi watakavyofanya kazi pamoja.

 

6.       Je ni kazi yake mahususi au ni part time job?

Mpiga picha wako hii ndio kazi yake mahususi inayomuweka mjini au ni hobbie tu, a part time thing to make extra money on the side? Hobbies, watu wengine wanachukulia hobbies zao na part time jobs very seriously na inawezekana isiwe tatizo, lakini uzoefu unaonesha kuwa watu huwa hawako serious na part time things, atakisogeza mpaka atakapoweza, kikwazo kidogo kikitokea haoni shida kuingia mitini na pesa na kazi yako. Nimepata hii experience first hand so sitanii. Make sure unafanya kazi na mtu serious, ideally iwe kampuni au studio na sio individual, wanaweza kuwa matapeli.

 

7.       Tabia yake je? Much know sana au anasikiliza mteja wake anataka nini?

Uzoefu unapoingia kichwani, unajaribu kumueleza mpiga picha idea zako kwasababu kuna vitu mahususi ungependa ambavyo sio vya kila siku nay eye anakwambia, “usijali niachie kila kitu, najua, najua si unataka wakati mnaingia….najua usijali” mmmh ujue huyo ameshakremu picha za kupiga, na ukija kuangalia album yako nay a kina Kiwanga ni the same pictures different people!! Unless huna makuu ukaamua kumuachia mpiga picha afanye kazi yake the best way anavyoijua, hakikisha mpiga picha wako anauwezo wa kucommunicate na kusikiliza matakwa yako na ayaelewe.

 

Kama ni Yule ambaye sio mzoefu na unafikiria kumpa chance, drop him now, kwasababu utamuelekeza na kumpa nyenzo zote za kumsaidia na yeye ataishia kufanya anachojua yeye, why? Hajasikia kitu chochote ulichosema, labda hata haelewi kuwa kupata hiyo kazi ukichukulia ukosefu wake wa uzoefu ni bahati, atakuharibia kazi yako!!

 

8.       Vifaa vya kazi na teknologia

Nitakubali kuwa mimi sio mtaalamu wa kamera na wasomaji wangu wengi vilevile, lakini ni vizuri kuhoji uwezo wa vifaa vya mpiga picha wako, anaweza kutoa picha nzuri usiku, mchana, kwa mbali karibu? Lakini walau awe na kamera yenye uwezo unaokubalika (will research some more) na vifaa vingine kama taa na milingoti yake.

 

Muhimu sana awe na packup set ya vifaa vyake in case anything goes wrong, wazoefu utaweza kuwatofautisha hapa kwasababu kwa wao huu ndio utaratibu wa kazi, feki watakua na kamera za kuazima bila backup ya aina yoyote.

 

9.       Kukabidhi kazi

Kazi ya picha mara nyingi huwa tayari hata siku inayofuata kama zitaenda studio moja kwa moja, hata hivyo wiki moja ni muda wa kutosha kwa mpiga picha wako kuwasilisha kazi yako. Ana uwezo huo? Mkubaliana kazi itakua tayari baada ya muda gani.

 

Kazi itawasilishwa katika media ipi? Hard copies ndani ya album? Bila album? Na CD au la? Picha ngapi, size gani? Album ngapi? Lazima mkubaliane ili kusiwe na lawama mwisho wa siku.

 

10.   Je unapata Value for your money?

Hiki ni kitu muhimu sana ambacho watu wengi huwa kinawapita bila wao kujua. Kuna wapiga picha wanauza majina, in which case wanakupumbaza na wewe unafeel chochote watachosema lazima ndio chenyewe. Sio kweli siku zote, mara nyingi wapiga picha wenye majina huwa wako in demand sana na huwa wanashawishika kuchukua kazi nyingi kwa wakati mmoja, hawachelewi kukuahidi kila kitu and then siku ya siku wanakutumia mtu baki, utafanya nini? Siku ndio imeshafika, umeshatumia muda wako mwingi kumake sure things go right ghafla kitu kama hiki kinatokea.

 

Niamini nitakapokuambia kuwa kuna wapiga picha bora sana ambao hawana majina, na ukifuata hizi hatua utaweza kuwagundua baadhi. Hawa watakua na gharama nafuu lakini watakufanyia kazi ambayo otherwise ungelipa mapesa na mapesa kwasababu tu ya jina.

 

Basically kama mpiga picha amepasi hizo hatua hapo juu then ataweza kukufanyia kazi itakayokuridhisha, hata kama gharama yake haitakua nafuu kihivyo, atakua muadilifu na muaminifu, so make sure you get value for you money, quality and peace of mind is what you want so you can relax on your day.

 

Sio muhimu sana lakini bonus kama mpiga picha huyu na timu yake watavaa nadhifu siku hiyo, sio mbaya kutinga suti hivi so akablend na wageni.

 

Mwisho nasemaje, tujenge tabia ya kuwa tunasign mikataba na hawa watu, wengi wanataka malipo yote up front, au nusu ya kumbook, nusu siku ya harusi shughuli inapoanza, akiharibu kazi au asipokuridhisha ni wachache wenye ustaarabu wa kusema wakurefund pesa zako kwa kuwa wameshindwa kudeliver as expected, wengi watakuyeyusha utabaki unasononeka with nothing to hold this guy against, huna picha au mbaya na pesa umelipa. Mikataba inabidi ieleze vema nini kinategemewa kustahili malipo, na kwasababu harusi ni siku isiyorudia, akiharibu kazi inabidi akulipe fidia, hii itawafanya wapiga picha kuwa makini zaidi katika kazi zao, au unasemaje? Nitawawekea templates za mikataba siku za usoni.

Author: Mary
Date: 2008-11-03 00:00:00
What other people think...!
Unadhani ni upigaji au na mistudio ya bongo uchwara ndo mana wengi sikuhizi wanapenda eti wakapige picha japo moja photo point?! halafu picha za photopoint zinanichufua sasa mana background ni zile zile iweje hivyo hivi nao ni uchwara?
JJ 2008-11-06
mm sikubaliani na kusema na wao ni uchwara ila nafikiri wanatia ubahiri kwani pesa wanapata lkn hawataki ku-update resourse zao na vilevile wabongo wnapenda sana kuigana hawajui kua unaweza kuchagua venue yyt nzuri na ukapiga picha kwa pozi tofauti na zikawa bomba sana sio lazima photo point.tujifunze kuwa wabunifu hata ss wenyewe tusisubili kutengenezewa kila ki2, we angalia kwenye albamu za humu karibu picha nyingi sana zinafanana tofauti ni watu tu kama alivyosema mwandishi mm nafikiri tunahitaji mageuzi katika fani hii ya upigaji picha.
Joyce Mahila Khosla 2008-11-17
Joyce Mahila Khosla! Ingesaidia sana endapo kama ungefafanua zaidi ni mageuzi gani 'tunahitaji' katika fani ya upigaji picha. Haumtendei mtu haki kudai mageuzi bila kutaja ni mageuzi ya aina gani, hasa ikizingatiwa wewe si msemaji wa kila mtu, na pia hujaainisha nini unachotaka. Nawe JJ 'unayechufuka' na picha za photopoint, ina maana jamii yote inaishi chini ya paa moja, yaani kila picha inaanikwa kuonekana na kila mtu? Mbona huhoji kwa nini CocaCola isiwepo vinginevyo? Ama kwa nini askari hawabadili magwanda? Ama kwa nini kuna usiku na mchana daima milele? Unapozungumzia ubahiri (Joyce) unatakaje kwani? Ni wapi ulikoona kuna background zaidi ya hizo zilizopo photopoint. Simaanishi hakuna umuhimu wa kubadilisha, lakini je umeshaomba ukapigiwe mahali kama ufukweni ama bustanini ukakataliwa? Ama hizo background ziondolewe picha ipigwe chukuchuku?
issamichuzi@gmail.com 2009-01-04
je ni lazima kwenda kupiga picha mbali na ulikofungia harusi?picha za nyumbani hata iwe kijijini hazitoshi?niondoeni ushamba.
lkisota@iaa.ac.tz 2009-01-06
jamani jamani dada joyce! mimi nakubaliana na michuzi hapo juu (ingawa sijui kama bw. issa amejitetea kibiashara) ni kwamba kuhusu venue na background kufanana ni ubahari wetu sisi maharusi. hivi dada joyce unajua kama photo point wanapiga picha hata kanisani, msikitini, nyumbani na hata ukumbini? mimi sijaoa, lakini nishaudhuria vikao vingi vya harusi na cha mwisho ni cha jamaa yangu (wenyewe tunaita mshkaji). tuliweza kuwapigia photo point while tupo kwenye kikao na walitueleza hayo masuala hapo juu.tofauti ni gharama ndugu zangu. kama ujavyo wale jamaa ni proffesional na kulingana na ukweli huo lazima wae na gharama ukilinganisha na juma au hussein mpiga picha pale magomeni. jamaa walikua tayari kupiga picha home, msikitini na hata ukumbini achilia mbali beach sijui hotelini. sasa kaka wanaweza kupiga picha katika location hizo hapo juu, je kweli background zitafanana kweli. zitafanana kwa sisi tunaoenda pale studio zao myfair ground kwani wote tutakalia kile kigoda na ile sticker kule nyuma itokee (though ki- IT unaweza kubadili ile background lakini tatizo litabaki palepale, gharama) kama tatizo si gharama au ubahili kama ulivyouta dada joyce basi watu tungetoa pesa then photo point wangekuja bustanini na tukaweka pozi za kutosha jamaa wakaziprocess na kuprint hizo picha katika mitambo yao ya kisasa na kupendeza. mwisho kabisa naomba pia niweke wazi jambo hili. photopoint wako kibiashara zaidi. na kila mfanyabiashara lazima aangalie faida (hiyo ndio dhima kubwa ya biashara) na faida ni kureduce production cost na kuuza kwa price kubwa kulingana na value ya product husika. sasa ndugu yangu ukitaka ubadilishiwe background kwa kila harusi ili zisifanane backround je hapo photo point watakua wanapunguza au wanaongeza production cost? na je kwa style hiyo watakua wanamake profit au wanamake loss? ni kahome wake kadogo tu ambacho naamini utakafanya.asante!
elfather@yahoo.com 2009-01-15
   
Comment
Email/Name
Code
 
 
   
 
 
 
 
<<Back to Articles<< >>
womens pants, wedding dresses, wedding pictures, women shoes, wedding accessories, women nails, women hair, women message women send off, good wedding shoes and hotels
Any use of materials or photographs from HarusiYangu is strictly prohibited
© 2007. All Rights Reserved Designed and maintained by Bomba Designs